Posts

Simu za Samsung Galaxy Note 7 ni marufuku Tanzania

Image
Image copyright GETTY IMAGES Image caption Samsung imesema haitaunda tena simu aina ya Galaxy Note 7 Tanzania na Rwanda zimepiga marufuku uingizaji, usambazaji na utumiaji wa simu za Samsung aina ya Galaxy Note 7. Hatua hiyo imechukuliwa baada ya visa vya simu hizo kulipuka na kushika moto kuripotiwa nchi mbalimbali, jambo lililoifanya kampuni hiyo kutangaza haitaunda tena simu hizo. Aidha, Samsung iliwashauri wote waliokuwa wamenunua simu hizo kuzizima na kutozitumia tena. Nchi hizo mbili za Afrika Mashariki zimefikia uamuzi huo katikati ya wiki iliyopita huku nchi nyingine kama Kenya zikisema hatua ambazo kampuni ya Samsung imezichukua hadi sasa zinatosha. Samsung: Zimeni simu za Note 7 ni hatari Rwanda yapiga marufuku Galaxy Note 7 Kwa mujibu wa gazeti la The East African, Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano TanzaniaBw Innocent Mungy, amewataka wananchi wote ambao wamenunua simu hizo kuzizima na kuzirudisha katika maduka waliyonunulia na wauzaji hao kufuat...

VANESSA ALIVYOTUMBUIZA MOMBASA

Image

STAN BAKORA. VIDEO NISAMEHE

Image

ALLI KIBA KUAKATIZA SHOW YA MOMBASA

Image

SUGUA BENCHI. MATONYA NEW VIDEO

Image

Alikiba na Vanessa Mdee kutumbuiza na Chris Brown Mombasa

Image
Wawili hao watatumbuiza pamoja na Chris Brown, Oktoba 8, mwaka huu kwenye tamasha la Mombasa Rocks Music. “Mombasaaaaaa it’s ME N U this weekend. @mombasarocksfestival   #Juu #Niroge,”  ameandika Vanessa kwenye Instagram. Nyota wa Nigeria, Wizkid naye atatumbuiza kwenye tamasha hilo kubwa

Alikiba na Vanessa Mdee kutumbuiza na Chris Brown Mombasa

Image
Wawili hao watatumbuiza pamoja na Chris Brown, Oktoba 8, mwaka huu kwenye tamasha la Mombasa Rocks Music. “Mombasaaaaaa it’s ME N U this weekend. @mombasarocksfestival   #Juu #Niroge,”  ameandika Vanessa kwenye Instagram. Nyota wa Nigeria, Wizkid naye atatumbuiza kwenye tamasha hilo kubwa

Mwamko wa wasichana katika teknolojia Tanzania

Image
Hauhitaji Media Player Pata usaidizi kuhusu Media Player Bonyeza 'Enter' kuendelea au kurejea mwanzoni Mwamko wa wasichana katika teknolojia Tanzania 30 Septemba 2016 Azma yao ni kufundisha wasichana wengi iwezekanavyo maswala ya teknolojia. Kuandika programu za kompyuta na simu, kutengeneza programu tumishi na hata kubuni na kutengeneza mitandao. Wakiwa wameanza miaka mitatu tu iliyopita, Apps & Girls ni shirika lisilo la kiserikali ambalo tayari limewafikia wasichana zaidi ya 600 kupitia mtandao wa shule za sekondari takribani 17. Mwanzilishi wa Apps & Girls Carolyne Ekyarisiima amezungumza na BBC kuelezea wanafanyaje kuongeza mwamko wa wasichana katika teknolojia nchini Tanzania.
Image
Mzozo Kashmir: Pakistan yapiga marufuku filamu za India Image copyright AP Image caption Filamu za Bollywood zinazowashirikisha waigizaji maarufu kama Deepika Padukone, kulia, ni maarufu sana Pakistan Majumba makuu ya cinema nchini Pakistan yamepiga marufuku filamu za India, kama ishara ya kuonyesha umoja wao na vikosi vya Pakistan katika mzozo unaoshuhudiwa katika eneo la Kashmir. Marufuku hiyo imetangazwa katika miji ya Lahore, Karachi na Islamabad. Hatua hiyo inafuatia mzozo unaozidi kutotkota kati ya India na Pakistan. Siku ya Ijumaa, watayarishaji wa filamu kutoka India walipiga marufuku waigizaji wa Pakistan kufanya kazi Bollywood. Mwanasiasa mmoja wa mrengo wa kulia, amewaamrisha waigizaji wa Pakistan kuondoka India. Mhariri wa BBC kusini mwa bara Asia Charles Haviland anasema kwamba sio mara ya kwanza ambapo mzozo kati ya India na Pakistan umeathiri utamaduni wa mataifa hayo mawili. Mwandishi wa BBC anasema filamu za India ni maarufu sana Pakistan, kwani sekt...

Mji wa Aleppo washambuliwa tena

Image
Image copyright REUTERS Image caption Hospitali hiyo pia ilishambuliwa mapema wiki jana. Mashambulizi ya angani yanayoendelea katika mji unaoshikiliwa na waasi wa Allepo nchini Syria, yamegonga hospitali. Kundi la Syrian American Medical Society, linalofadhili hospitali hiyo linasema kwamba hospitali hiyo ilishambuliwa kwa makombora mawili. Hospitali hiyo pia ilishambuliwa mapema wiki jana. Ripoti zinaibuka kwamba vikosi vinavyoungwa mkono na Urusi pamoja na vikosi vya Syria vinashambulia mji wa kale wa Allepo, na kukabiliana na waasi katika mitaa mbalimbali. Image copyright REUTERS Image caption Mji wa Aleppo umekumbwa na uharibifu mkubwa

(AUDIO) DIAMOND Platnumz Kwenye Remex . HATA NIKILA WOTE DINI YANGU SIO DHAMBI

Image
(AUDIO) DIAMOND Platnumz Kwenye Remix Hii Nyingine na Kawataja Wema Sepetu, Hamisa Mobeto na Zari Bonyeza Play Hapa Chini:

Samsung kuuza tena Galaxy Note 7

Image
Image copyright AFP Image caption Takriban simu, Galaxy Note 7, milioni mbili laki tano zilirejeshwa kutoka maeneo mbalimbali ulimwenguni, ili kupata btari mpya. Samsung imeanza mauzo ya simu yake, Galaxy Note-Seven nchini korea kusini, baada ya kusitisha mauzo yake mwezi mmoja uliopita, kutokana na madai kwamba simu hizo zinalipuka. Kampuni hiyo inasema hitilafu kwenye batri zake zilisababisha milipuko hiyo. Takriban simu milioni mbili laki tano zilirejeshwa kutoka maeneo mbalimbali ulimwenguni, ili kupata btari mpya. Makampuni ya usafiri wa ndege yamekuwa yakiwaonya wateja wake dhidi ya kutumia simu hiyo ndani ya ndege. Hata hivyo sio simu zote zilizo na hitilafu kwenye batri zilizorejeshwa, na hivyo haijulikani wazi wakati marufuku ya kutumia simu hizo ndani ya ndege itakapoondolewa. Samsung inatoa simu za bure kwa wale walioathirika huku wafanyibiashara wa simu hizo wakipata mali mpya huku simu zaidi zikiendelea kufikishwa sokoni ''Tumetoa wito kwa waathiri...

Wenger: Wachezaji wa Afrika wamenifaa sana katika soka

Image
Image copyright GETTY IMAGES Image caption Arsene Wenger ameongoza Arsenal kwa miaka 20 Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ameiambia BBC kuwa wachezaji kutoka nchi za Afrika wamekuwa wenye umuhimu mkubwa katika taaluma yake ya miaka 20. Wenga alikuwa akizungumza wakati wa mkutano wake wa kawaida na waandishi wa habari kabla ya mechi ambapo pia alitunukiwa kwa kukiongoza klabu hicho kwa miongo mwili. Image copyright GETTY IMAGES Image caption Nwankwo Kanu wa Nigeria alikuwa mmoja wa wachezaji waliokuwa wenye umuhimu mkubwa kwa Arsene Akiwa mwenye uso uliotabasamu, Wenger amesena kuwa wachezaji kutoa Afrika wana moyo, wenye ubunifu na nguvu, masuala ambayo ni vigumu kuyapa kwenye mchezo. Aliwataja wachezaji akiwemo Nwanko Kanu wa Nigeria, Kolo Toure wa Ivory Coast na gwiji raia wa Liberia George Weah, ambaye alikuwa meneja wake katika klabu ya Monaco nchini Ufaransa, kama wachezaji watatu waliokuwa na uswawishi mkubwa katika taaluma yake. Image caption Wenger akihutubia wanahabari...

Video ya raia wa Uganda akiuwawa na polisi Marekani yatolewa

Image
Polisi katika mji wa Marekani San Diego wametoa mkanda wa video ya mwanamme mweusi aliyepigwa risasi na kuuwawa na polisi siku ya jumanne. Image copyright REUTERS Image caption Waandamanaji, akiwemo Bi Agnes Hassan (aliyejifunga kitambaa kichwani), wakilalamikia kuuawa kwa Olango Video hiyo inaonyesha maafisa wawili wa polisi wakimkaribia Alfred Olango - mkimbizi kutoka Uganda - ambaye hakuwa amejihami, kabla ya mmoja wao kumfyatulia risasi katika mtaa wa El Cajon. Polisi wanasema kwamba mwanamme huyo alionyesha tabia potovu isiyoeleweka, japo mamake mzazi anasema alikuwa na matatizo ya kiakili na alifaa kupata usaidizi. Tukio hilo lilisababisha maaandamano makali katika eneo la El Cajon. Polisi huyo anaonekana akifyatua risasi mara nne, baada ya mwanamme huyo kuinua mikono yake hadi kwenye eneo la kifua, ishara ambayo polisi wanasema ilikuwa ya kujitayarisha kufyatua risasi. Video hiyo imetolewa baada ya siku tatu za maandamano makali , na katika mkesha wa siku ambayo famil...

Video ya raia wa Uganda akiuwawa na polisi Marekani yatolewa

Image
Polisi katika mji wa Marekani San Diego wametoa mkanda wa video ya mwanamme mweusi aliyepigwa risasi na kuuwawa na polisi siku ya jumanne. Image copyright REUTERS Image caption Waandamanaji, akiwemo Bi Agnes Hassan (aliyejifunga kitambaa kichwani), wakilalamikia kuuawa kwa Olango Video hiyo inaonyesha maafisa wawili wa polisi wakimkaribia Alfred Olango - mkimbizi kutoka Uganda - ambaye hakuwa amejihami, kabla ya mmoja wao kumfyatulia risasi katika mtaa wa El Cajon. Polisi wanasema kwamba mwanamme huyo alionyesha tabia potovu isiyoeleweka, japo mamake mzazi anasema alikuwa na matatizo ya kiakili na alifaa kupata usaidizi. Tukio hilo lilisababisha maaandamano makali katika eneo la El Cajon. Polisi huyo anaonekana akifyatua risasi mara nne, baada ya mwanamme huyo kuinua mikono yake hadi kwenye eneo la kifua, ishara ambayo polisi wanasema ilikuwa ya kujitayarisha kufyatua risasi. Video hiyo imetolewa baada ya siku tatu za maandamano makali , na katika mkesha wa siku ambayo famil...